Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo – TBA, Arch. Elius Mwakalinga akimkabidhi Mkataba wa Makubaliano ya mradi wa ujenzi wa nyumba 320 Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa. Hafla hiyo ya uwekaji saini makubaliano hayo ya ujenzi wa nyumba za askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Dar es Salaam imefanyika leo Desemba 19, 2016 Jijini, Dar es Salaam katika Ukumbi wa TBA. Ujenzi wa nyumba hizo ni agizo la Rais Magufuli kufuatia ziara yake hivi karibuni ambapo alitoa kiasi cha bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za makazi ya askari wa Jeshi hilo.

 

Kwa habari picha zaidi tembelea www.magereza.blogspot.com