Kamishna Jenerali wa Magereza - CGP. John Casmir Minja(katikati) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Majengo, Bw. Elius Mwakalinga wakiangalia moja ya eneo la Gereza Segerea ambalo litajengwa nyumba za kuishi za Maafisa na askari wa Jeshi hilo(kushoto) ni Mkuu wa Gereza Kuu Segerea, ACP.  Godfrey Kavishe akiwaonesha eneo hilo walipofanya ziara ya kukagua maeneo mbalimbali ya Jeshi ambapo tayari Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa Bilioni 10 kwa Jeshi la Magereza kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Maafisa na askari wa Jeshi hilo katika Mkoa wa Dar es Salaam.

 

Kwa habari picha zaidi tembelea www.magereza.blogspot.com