Na Mwandishi Wetu
Jeshi la Magereza nchini limeokoa jumla ya Shilingi Bilioni 11, ikiwa ni gharama ya chakula cha wafungwa tangu lianze kujitegemea kwa chakula ikiwa ni maelekezo ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kulitaka jeshi hilo litumie nguvu kazi ya wafungwa ilionao kuzalisha chakula.
Akizungumza leo katika ziara ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,iliyofanyika katika Makao Makuu Mapya ya Jeshi hilo ,Msalato jijini Dodoma, Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee amesema walikuwa wanatumia Shilingi Bilioni Moja kila mwezi kulipa wazabuni wa chakula waliokuwa wanaliuzia chakula jeshi hilo.
“Sasa hivi tunajitegemea asilimia kubwa kwa chakula, Serikali kabla ya mwezi wa tatu mwaka jana kila mwezi kulikua kuna deni la Bilioni Moja, lakini baada ya mwezi huo wa tatu sasa tunaokoa kiasi hicho cha fedha shilingi bilioni moja na mpaka sasa tuna miezi kumi na moja tunajilisha wenyewe kupitia shirika la magereza” alisema CGP Mzee
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Naibu Waziri, Khamis Hamza Chilo alilipongeza Jeshi la Magereza kwa kutekeleza vyema agizo la Rais Magufuli ikiwa sambamba na ujengaji wa kiwanda kikubwa cha samani ambapo mpaka kukamilika kwake kitagharimu shilingi Bilioni 1,101,743,123/=
“Niwapongeze kwa hatua mbalimbali za maendeleo ambazo zingine nimeshuhudia mwenyewe,lakini kubwa kuweza kujitegemea kwa chakula cha wafungwa hali iliyopelekea kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambacho kinabaki humu humu ndani na mnakitumia kwa shughuli zingine za maendeleo hongereni sana” alisema Naibu Waziri Chilo
HABARI MPYA | Habari zaidi |
-
TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI JESHI LA MAGEREZA TANZANIA BARA
12-04-2024
Bofya hapa ili kupata orodha hiyo.
-
TANGAZO LA AJIRA JESHI LA MAGEREZA TANZANIA BARA
09-01-2024
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara anatangaza nafasi za Ajira za kujiunga na...
-
CGP.NYAMKA AFUNGA KOZI NAMBA 12 YA ASKARI WA KIKOSI MAALUM.
02-11-2023
KAMISHNA Jenerali wa Jeshi la Magereza CGP. Mzee Ramadhani Nyamka Oktoba 27, 2023 amefunga Mafunzo...
-
TANGAZO LA KUITWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA AWALI YA JESHI LA MAGEREZA
04-08-2023
Kupata Orodha ya Majina hayo bonyeza...
-
KUITWA KWENYE USAILI JESHI LA MAGEREZA TANZANIA BARA
20-06-2023
Tangazo la kuitwa kwenye usaili Jeshi la Magereza Tanzania Bara bofya hapa kupata orodha ya majina...
-
FOMU YA KUJIUNGA NA CORRECTIONAL SCIENCE
17-05-2023
Chuo cha TCTA kinatangaza nafasi za kujiunga na chuo, kupata fomu bofya...
HISTORIA YA JESHI LA MAGEREZA TANZANIA BARA |
1.0.Utangulizi Jeshi la Magereza lilianzishwa rasmi mwezi Agosti 25,1931 baada ya mgawanyo wa majeshi ya Polisi na Magereza kutokea. Licha ya kuwa na majukumu ya kulinda usalama na mali za wageni, kabla ya mwaka 1931 Jeshi la Polisi lilifanya pia kazi za Magereza kama zilivyokuwa kwa tafsiri na madhumuni ya wakoloni. Jeshi la Magereza wakati lilipoanzishwa liliitwa Idara ya Jela ambapo shughuli zake zilibaki kuwa zile za kikoloni za utesaji wa wafungwa pamoja na kazi ngumu bila kujali kama ni ya manufaa kwao au kwa Taifa. Dhima ya Jeshi la Magereza ni kutekeleza wajibu ipasavyo katika kuimarisha ulinzi wa jamii kupitia usimamizi wa kifungo na kuwasimamia wahalifu, huduma za mahabusu, programu na huduma zinashughulikia mahitaji ya urekebishaji wa wahalifu na ushauri wa Sera kuhusu uzuiaji wa uhalifu na ushughulikiaji wa wahalifu. Soma zaidi>> |